Loading...

HABARI NZITO...MKUTANO WA GHAFLA ULIOITISHWA NA RAIS MAGUFULI NA VIGOGO WAZITO WA CCM WAIBUA MAPYA ILA KUBWA ZAIDI NI HILI LA "MAJIPU YATAONDOKA NA CCM"

▼▼▼TO SEE PHOTOS AND THE VIDEO CLICK HERE DOWN▼▼▼
John Magufuli, Rais wa Tanzania (kulia) akiwa na Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete
WIKI iliyopita, Rais John Magufuli aliitisha mkutano wa ghafla kukutana na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ngazi ya mikoa na wilaya zote nchini, anaandika Ansbert Ngurumo.
Mwaliko huo ulikuwa wa ghafla na uliambatana na sharti moja kuu la viongozi hao kutofika Dar es Salaam wakiwa wamevaa sare za chama.
Gharama za safari zililipwa na Ikulu na makada hao waliondoka wakifurahia jinsi Ikulu ilivyowakarimu kwa chakula safi, kingi na cha kusaza!
Mkutano huo ulifanyika Ikulu na ilionekana wazi kuwa, waandaaji walikuwa ni maofisa wa Ikulu. Abdulrahmani Kinana, Katibu Mkuu na vijana wake wa makao makuu, hawakuwa na raha.
Walionekana wazi kuchoka na kusubiri mkutano huo uishe ili waendelee na shughuli zake nyingine.
Baada ya kufika katika ukumbi wa mkutano huo, hata itifaki za kawaida za mikutano ya ndani ya CCM zilikuwa hazieleweki, jambo lililomfanya Kinana kusimama mara kadhaa kurekebisha hapa na pale ili mambo yaende.
Kinana alikuwa na ujumbe mmoja kwa washiriki – kwamba mwezi Juni mwaka huu, Rais Magufuli atakabidhiwa chama kama mwenyekiti.
Kabla ya mkutano huo, nje ya ukumbi wa mikutano Ikulu na kwenye hoteli walikofikia makada, gumzo kuu lilikuwa ni kama CCM itakuwa salama chini ya Magufuli.
Wapo waliojidanganya kuwa Jakaya Kikwete, mwenyekiti wa sasa, hawezi kukabidhi chama mpaka 2017. Mashabiki hao wa Jakaya walisema Rais Magufuli aachwe aendelee na kazi ya kutumbua majipu serikalini, chama kibaki na Jakaya, ili kibaki salama.
Pale ukumbini, baada ya Kinana kutangaza kuwa Rais Magufuli atakabidhiwa chama mwezi Juni, kundi dogo la makada mashabiki wa Magufuli walishangilia, huku wakijishtukia wenyewe kwa wenyewe.
Walio wengi hawakuona sababau ya kushangilia kwa sababu kwanza ni utaratibu wa kawaida kufanya hivyo, na pili, kushangilia ni sawa na kusema wamechoka na uongozi wa Jakaya.
Baada ya mgongano ya kiitifaki, Rais Magufuli alipata nafasi ya kuwahutubia. Kwa kusudi la makala hii nitataja machache ya aliyozungumzia.
Kwanza, alisema amewaita viongozi hao kuwashukuru kwa kumpigania hadi akachaguliwa kuwa rais. Alikiri kuwa bila wao, asingekuwa hapo alipo. Pili, aliwaeleza kuwa amewaita kuwahakikishia kuwa nchi iko salama na chama kitakuwa salama.
Tatu, alisema amewaita kuwahakikishia wale wenye mashaka na kasi yake ya utumbuaji majipu, na walioanza kupinga hatua hizo waache kumkatisha tamaa. Akatumia muda mrefu kueleza baadhi ya hisia zinazoenezwa kuwa anakiuka haki za binadamu, kuwa mizigo bandarini imepungua, na kuwa atadhalilisha CCM.
Mpaka hapa kuna mambo mawili makuu ya kutazamwa kwa umakini. Kwanza, Rais Magufuli alifanya kampeini kwa kusisitiza, “Tanzania ya Magufuli” itafanya hili na lile. Alikuwa mwangalifu sana kutotanguliza CCM mbele ya umma uliokuwa umekata tamaa na CCM.
Hata baada ya kuapishwa, mara mbili ametofautiana na Kikwete katika vikao vya kamati kuu. Mara ya mwisho walitofautiana kuhusu suala la uchaguzi wa Meya wa Jiji la DSM.
Katika kikao hicho, baadhi ya wajumbe wa kamati kuu walilalamika kuwa kuna mawaziri na watumishi wa serikali wanashabikia uchaguzi ufanyike na meya atoke Ukawa (Umoja wa Katiba ya Wananchi).
Kikwete aliunga mkono na kutaka hatua zichukuliwe dhidi ya wote walio serikalini na wanashibikia jiji liende Ukawa. Kabla ya kuhitimisha ajenda hiyo, Rais Magufuli akaomba kuzungumza.
Katika mchango wake, akakiri kuwa wapo wanaounga mkono na yeye ni mmoja wao. Akasema kama ni kosa lilifanyika pale CCM iliporuhusu uasi ndani yake na kusababisha mkoa wa Dar es Salaam uwe na madiwani wengi wa Ukawa.
Akakumbusha kuwa hata yeye wakati wa kampeni alifika mahali akaacha kwenda kwenye vikao vya usiku vya kufanya tathmini ya kampeini kwa sababu ya fitina na uasi.
Akasisitiza kuwa kama CCM haitaacha majungu, yeye hatakuwa tayari kuitetea. Akahitimisha kwa kusema, ni vizuri “tuwaache Ukawa watutawale Dar es Salaam ili tuonje uchungu wa kutawaliwa kwa sababu ya uasi wetu”.
Baada ya mchango wa Magufuli, Jakaya Kikwete aliahirisha kikao kwenda kunywa chai. Mgongano huu wa Kikwete na Magufuli hauwezi kuiacha CCM ikawa salama.
Hii ni kwa sababu huwezi kusifia hatua anazochukua Magufuli bila kulaani uongozi wa Jakaya. Mpaka sasa Magufuli hajaanzisha jambo jipya serikalini, bali anachofanya ni kukosoa utendaji wa Rais Kikwete.
Kwa hiyo, tangazo kwamba Magufuli atakabidhiwa CCM mwezi Juni si tangazo la heri kwa CCM ya Kikwete. Ni tangazo la kutumbua majipu ndani ya CCM yakiwamo yale yaliyomwezesha Magufuli kuingia madarakani.
Hata kama Magufuli anatamba hadharani kuwa hakuna mfanyabiashara yeyote aliyemchangia hata senti moja, lakini CCM na vyombo vyake vilifanya madudu makubwa kumwezesha Magufuli “kushinda” urais.
Matajiri walichangia CCM iliyokuwa inamnadi yeye. Je, yuko tayari kufumua hata jipu hilo?
Jambo la pili ni ukweli kuwa majipu anayoyatumbua Magufuli si ya wapinzani bali watendaji wa serikali ya CCM. Kwa hiyo, majipu yanayotumbuliwa ni matawi lakini. Mashina ya majipu ni CCM.
Je, uking’oa shina mti utapona? Huu ndiyo wasiwasi unaoikumba CCM ikiwa mikononi mwa Magufuli. Kwa hiyo, wana CCM wanaoijua CCM wanajua kuwa CCM haitakuwa salama, ingawa yeye aliwahakikishia kuwa itakuwa salama.
Kwanini alilazimika kuwahakikishia usalama? Magufuli anaishi kwenye nadharia kuwa mafisadi ndani ya serikali na ndani ya chama, hawakutumwa na chama kufanya uchafu.
Magufuli anaishi katika njozi kuwa anaweza kutumbua majipu yaliyo katika sehemu nyeti – tena bila ganzi – halafu mgonjwa akabaki kuchekelea na kushangilia.
Wenye hekima na wazee wa chama wanajua majipu mengine yameumbwa ndani ya CCM, na ndiyo yanashikilia uhai wa CCM. Ukiyatumbua, umeitumbua CCM. Hata kwa hekima ipi, hayatumbuliki. Na yakitumbulika, yanaondoka na CCM.
Ufisadi wa mabilioni na mikataba feki ndiyo imeifikisha CCM na serikali yake hapa ilipo. Hata kwa kitendo cha Magufuli kuita makada wa CCM kwa kutumia fedha ya serikali wakati akidai kubana matumizi, tayari ametengeneza kipere kitakachogeuka jipu.
Uzoefu pale Ikulu na Lumumba – makao makuu ya CCM – ni kuwa mikutano ya namna hiyo hutumia mara tatu ya gharama halisi.
Hiyo ndiyo CCM atakayokabidhiwa Magufuli mwezi Juni. Magufuli hajui CCM. Kama angeijua, asingeikaribisha Ikulu kwa ajili tu ya kuihakikishia kuwa itakuwa salama yake.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright bongonews | Designed By JAMIIYETUBONGO.COM
Back To Top